Thursday, 3 November 2016

MADRID YA KOMALIWA UEFA


 Klabu bingwa barani Ulaya imeendelea usiku wa kuamkia leo ikiwa bado katika hatua za makundi.
Mchezo wa kusisimua zaidi ukiwa kati ya Legia Warsaw dhidi ya

Wednesday, 2 November 2016

MAN CITY YAIGARAGAZA BARCELONA

UEFA: Manchester City wapata ushindi wa kusisimua dhidi ya Barcelona


manchester City celebrate
Manchester City wanahitaji kushinda mechi moja kufika hatua ya muondoano Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya baada ya kupata ushindi wa kusisimua dhidi ya miamba wa Uhispania Barcelona.

Wednesday, 19 October 2016

TAZAMA JINSI GUADIOLA ALIVYO KARIBISHWA ENGLAND


VIDEO JINSI CHELSEA ILIVYO IADHIBU LEISTER CITY KWENYE EPL


ANGALIA GOLI LA KICHUYA DHIDI YA YANGA


Tennis: Kyrgios afungiwa kucheza wiki nane

Na Salama Ngale

Muaustralia Nick Kyrgios amefungiwa kwa wiki nane na kutozwa faini ya dola za kimarekani 25,000 kwa utovu wa nidhamu-ikiwa ni pamoja na kucheza ovyo wiki iliyopita michuano ya Shaghai Masters.

Nick mwenye miaka 21 amekuwa akigongesha mpira juu ya wavu mara kadhaa katika mchezo aliofungwa Mischa Zverev kwa seti 6-3 6-1 .
Mchezaji huyo nambari 14 kwa ubora duniani ameomba radhi kwa tukio hilo na kusema atafanyia kazi wakati huu akiwa kifungoni.
Wiki iliyopita Muingereza Andy Murray alisema hafikirii kuwa faini pekee itakuwa adhabu tosha.
Mwaka 2015 Kyrgios alifungiwa siku 28 na faini ya dola 25,000 baada ya kutoa maneno ya kashfa kwa mpenzi wa Stan Wawrinka katika michuano ya kombe la Rogers.

TAKWIMU ZAMBEBA KIPA SIMBA, ASHIKILIA USUKANI WA KIPA BORA


VICENT
Na salama Ngale 
Kipa wa Simba, Vincent Angban mpaka sasa ndiye aliyecheza mechi nyingi bila kuruhusu bao ‘clean sheet’, akifanya hivyo kwenye michezo sita kati ya tisa iliyocheza Simba huku akisimama golini mechi zote, sawa na dakika 810.

Muivory Coast huyo aliyetoswa na Azam majaribioni mwanzoni mwa msimu kwa kile walichosema kiwango chake ni hafifu, mpaka sasa amefanikiwa kuiweka Simba kileleni mwa msimamo, huku akiwa ameruhusu mabao matatu tu katika mechi tatu pekee.

Simba inaungana na Yanga ambayo pia imeruhusu idadi hiyo ya mabao, ikiwa ni idadi ndogo zaidi, lakini tofauti ni kwamba lango la Yanga limelindwa na Deogratius Munishi ‘Dida’ na Ally Mustafa ‘Barthez’kwa nyakati tofauti.

Akizungumzia clean sheet, Angban alisema ni jambo la furaha kwake na shukrani kwa wachezaji wenzake pamoja na uwezo binafsi anayopigana kuhakikisha anauonyesha awapo uwanjani.

“Ni jambo zuri, lakini siku zote haya ndiyo matokeo ya mtu binafsi na timu kwa ujumla. Siwezi kusema kuhusu ni clean sheet ngapi nifikishe kwa sababu ninacheza kwa kujituma kwa ajili ya timu yangu ili iendelee kufanya vizuri,” alisema kipa huyo.

Mechi Simba ilizoruhusu bao ni katika ushindi wa 2-1 dhidi ya Ruvu Shooting, ushindi wa 3-1 dhidi ya Ndanda na sare ya 1-1 na Yanga, huku ikizikazia Kagera Sugar (2-0), Mtibwa Sugar (2-0), Majimaji (4-0), JKT Ruvu (0-0), Azam (1-0) na Mbeya City (2-0).

Wednesday, 12 October 2016

POGBA APIGA BAO LA MWENDO KASI UFARANSA IKIILAZA UHOLANZI BAO 1-0


Holland (4-3-3): Stekelenburg, Karsdorp, Bruma, van Dijk, Blind, Strootman, Wijnaldum (Dost 61), Promes (Depay 16), Morishige (Willems 83), Klaassen, Janssen.
Subs not used: Zoet, Veltman, de Vrij, Kongolo, Clasie, Toornstra, Vilhena, De Jong, Vorm
Booked: Strootman, Morishige  
France (4-2-3-1): Lloris, Sidibe, Varane, Koscielny, Kurzawa, Pogba, Matuidi, Sissoko, Griezmann (Kante 90), Payet (Martial 66), Gameiro (Gignac 79).
Subs not used: Mandanda, Laporte, Fekir, Kimpembe, Cabaye, Digne, Corchia, Coman, Areola.
Goal: Pogba 30

Booked: Pogba

HUYU TYSON FURY KIBOKO, KILA SIKU ANAIBUKA NA KITUKO KIPYA



Kati ya bondia anayeongoza kwa vituko kwa sasa ni Tyson Fury Wa Uingereza.
Mara atangaze kuwa

Argentina watandikwa Peru mechi ya kufuzu Kombe la Dunia



Mechi za Raundi ya 10 ya nchi za kanda ya Marekani ya Kusini chini ya Mwamvuli wa Shirikisho lao CONMEBOL kusaka nchi 4 zitakazotinga moja kwa moja huko Urusi Mwaka 2018 kwenye Fainali

Serge Aurier aokoa maisha ya mchezaji wa Mali


Beki wa klabu ya Paris Saint-Germain kutoka Ivory Coast Serge Aurier amesifiwa sana baada ya

Liverpool v Man Utd: Uteuzi wa refa Anthony Taylor wakosolewa



Image caption Mwamuzi Anthony Taylor alizaliwa Wythenshawe, maili 10kutoka uwanja wa Manchester United

Mkuu wa zamani wa marefa Uingereza Keith Hackett amekosoa uteuzi wa refa kutoka Manchester Anthony Taylor kuwa mwamuzi wa mechi ya Ligi ya Premia kati ya Liverpool na Manchester United.
Taylor huishi maili sita kutoka Old Trafford, na Hackett anaamini huenda hilo likasababisha madai wa kupendelea upande mmoja.
"Hakuna anayetilia sana uadilifu wake," Hackett alisema.
"Lakini je, kitu kikienda mrama? Itakuwa vigumu kwa baadhi kuvumilia."
Taylor hana uhusiano wowote na United lakini hushabikia klabu ya Ligi ya Taifa ya Kaskazini ya Altrincham.
Hackett anasema inashangaza ikizingatiwa kwamba Mark Clattenburg angepatikana siku hiyo ya Jumatatu.
Badala yake Clattenburg, ambaye ni shabiki wa Newcastle United, ataudumu kama mwamuzi wa nne mechi nyingine wikendi.
Tayari mashabiki wa Liverpool wameanza kulalamika mitandao ya kijamii kuhusu uteuzi wa Taylor.

Wednesday, 21 September 2016

DORTIMUND YAIVURUMISHA WOLFSBURG MABAO 5-1


Image copyright
Image caption




Borussia Dortmund imeonyesha haitaki utani kwenye Bundesliga baada ya kuichapa Wolfsburg mabao 5-1.S










HONGERA KILIMANJARO QUEENS KWA KOMBE LA CHALENJI

.

Na salama ngale
KIKOSI cha timu ya taifa ya wanawake ya Tanzania Bara, Kilimanjaro Queens, kimebeba kombe la Chalenji kwa

Tuesday, 13 September 2016

BEKI WA PREMIER LEAGUE APATA AJALI MBAYA YA GARI


Beki wa kushoto anayechea katika Ligi Kuu ya England 'Premier League' akiwa ni mchezaji wa timu ya Crystal Palace, Pape Souare amejeruhiwa katika ajali mbaya ya gari alipokuwa katika mitaa ya Jiji la Londo, ambapo ksa sasa yupo hospitali akipata

RONALDO APEWA UNAHODHA WA KIKOSI CHA REAL MADRID, AUNGANA NA WENGINE WATATU

Christian Ronaldo















Na salama ngale
Nyota Cristiano Ronaldo ametangazwa kuwa nahodha wa kikosi cha Real Madrid.

Ronaldo anachukua nafasi hiyo rasmi na kuwa mmoja wa manahodha wanne wa

Friday, 9 September 2016

MANCHESTER DERBY NI JUMAMOSI HII LAKINI THAMANI YAKE USIPIME!





Makocha Jose Mourinho wa Manchester United na Pep Guardiola wa Manchester City

Straika mkongwe wa Manchester United, Zlatan Ibrahimovic amefunguka mengi katika mahojiano marefu ya kwanza aliyoyafanya na kituo cha runinga na MUTV huku akigusia mchezo wa Manchester Derby dhidi ya Manchester City.


Guardiola sasa ni kocha wa Man City


Zlatan amesema kuwa anaamini yeye na kocha wake, Jose Mourinho wanaelewana falsafa kwa kuwa ni watu wa ushindi lakini alipoulizwa kuhusu Kocha wa Manchester City, Pep Guardiola alisema: “Nilikuwa namjua Guardiola wa Barcelona lakini huyu wa sasa simjui.”
 
Katika mahojiano hayo ambayo yamerushwa hewani leo Ijumaa, Zlatana amesema kuwa Guardiola ni kocha mzuri na alichokuwa akikijua kipindi cha nyuma kuhusu kocha huyo hawezi kusema ndivyo alivyo sasa.

“Kwa sasa simjui, kipindi kile kila mtu alijua ni kocha mzuri na nsiyo maana alifanikiwa, anafanyaje kazi leo, mimi sijui, anaendeleaje hilo nalo sijui kwa kuwa siyo kocha wangu,” alisema Zlatan.

TEMEKE YAANZA NA MOTO AIRTEL RISING STARS

Na Mwandishi Wetu, DAR ES SALAAM
PAZIA la michuano Taifa ya soka ya vijana chini ya umri wa miaka 17 ya Airtel Rising Stars jana lilifunguliwa katika uwanja wa Kukumbukumbu ya Karume jijini Dar es Salaam ambapo timu ya wavulana ya Temeke ilitoa onyo kali kwa timu shiriki kwa kuifunga Kinondoni 4-1.
Mchezo huo ulitanguliwa na mechi ya wasichana kati ya Arusha na Lindi ambapo Arusha waliibuka na ushindi wa 2-0. Magoli ya Arusha yalifungwa na Eva Michael dakika ya 39 kwa njia ya penalti na pili likifungwa na Warda Alfonce dakika ya 60.
Mchezaji wa Arusha, Diana Mosses (kulia) akiwania mpira na beki wa Lindi , Neema Hashim katika mashindano ya vijana ya Airtel Rising Stars kwenye Uwanja wa Karume jijini Dar es Salaam jana

Katika mchezo wa Temeke na Kinondoni, Temeke walianza kwa kasi ya aina yake na kupeleka mashambuliazi ya mara kwa mara langoni mwa Kinondoni huku Kinondoni wakionekana kuzidiwa katika kila idara.
Temeke waliandika bao la kwanza kupitia kwa Ramadhan Kawambwa kaika dakika ya 14, kwa njia ya penati baada ya mchezaji wa Temeke kufanyiwa madhambi katika eneo la hatari. Goli hilo lilipokelewa kwa shangwa na mashabiki wa Temeke.
Temeke awalipata bao lao la pili kupitia kwa Abirahi Uihuro mnamo dakika ya 34 ambaye aligongeana mpira kwa uzuri na Ismail Kovu na kisha kumchambua kipa wa Kinondoni kwa umaridadi wa hali ya juu na kuukwamisha mpira huo kimiani.
Mohammed Mbegu aliifungia Temeke bao la tatu katika dakika ya 40 na kuzidi kuzamisha jahazi la Kinondoni ambao walinekana kama vile wamesimama wakati mchezo ukiendelea.
Rosea Mpoma aliwaliza kwa mara nyingine tena Arusha baada ya kuifungia Temeke bao la tano katika dakika ya 53 baada ya kuachia shuti kali na kuzama moja kwa moja wavuni.
Alikuwa ni Abirahi Uihuro tena, ambaye aliiandikia Temeka bao la nne mnamo dakika ya 28 ya kipindi cha pili baada ya kuunganisha krosi iliyochongwa na Mohammed Mbegu kutoka upande wa kushoto mwa uwanja na kuendeleza karamu ya magoli kwa Temeke.
Kinondoni walipata goli ya kufuta machozi mnamo dakika 36, likifungwa na Shaban Mangula baada ya mabeki ya Temeke kushindwa kuokoa mpira wa kona.
Michuano hiyo ya Airtel Rising Stars itaendelea kesho kwenye uwanja wa Karume jijini Dar es Salaam na kufikia tamati Jumapili, Septemba 11.