Wednesday, 21 September 2016

DORTIMUND YAIVURUMISHA WOLFSBURG MABAO 5-1


Image copyright
Image caption




Borussia Dortmund imeonyesha haitaki utani kwenye Bundesliga baada ya kuichapa Wolfsburg mabao 5-1.S










HONGERA KILIMANJARO QUEENS KWA KOMBE LA CHALENJI

.

Na salama ngale
KIKOSI cha timu ya taifa ya wanawake ya Tanzania Bara, Kilimanjaro Queens, kimebeba kombe la Chalenji kwa

Tuesday, 13 September 2016

BEKI WA PREMIER LEAGUE APATA AJALI MBAYA YA GARI


Beki wa kushoto anayechea katika Ligi Kuu ya England 'Premier League' akiwa ni mchezaji wa timu ya Crystal Palace, Pape Souare amejeruhiwa katika ajali mbaya ya gari alipokuwa katika mitaa ya Jiji la Londo, ambapo ksa sasa yupo hospitali akipata

RONALDO APEWA UNAHODHA WA KIKOSI CHA REAL MADRID, AUNGANA NA WENGINE WATATU

Christian Ronaldo















Na salama ngale
Nyota Cristiano Ronaldo ametangazwa kuwa nahodha wa kikosi cha Real Madrid.

Ronaldo anachukua nafasi hiyo rasmi na kuwa mmoja wa manahodha wanne wa

Friday, 9 September 2016

MANCHESTER DERBY NI JUMAMOSI HII LAKINI THAMANI YAKE USIPIME!





Makocha Jose Mourinho wa Manchester United na Pep Guardiola wa Manchester City

Straika mkongwe wa Manchester United, Zlatan Ibrahimovic amefunguka mengi katika mahojiano marefu ya kwanza aliyoyafanya na kituo cha runinga na MUTV huku akigusia mchezo wa Manchester Derby dhidi ya Manchester City.


Guardiola sasa ni kocha wa Man City


Zlatan amesema kuwa anaamini yeye na kocha wake, Jose Mourinho wanaelewana falsafa kwa kuwa ni watu wa ushindi lakini alipoulizwa kuhusu Kocha wa Manchester City, Pep Guardiola alisema: “Nilikuwa namjua Guardiola wa Barcelona lakini huyu wa sasa simjui.”
 
Katika mahojiano hayo ambayo yamerushwa hewani leo Ijumaa, Zlatana amesema kuwa Guardiola ni kocha mzuri na alichokuwa akikijua kipindi cha nyuma kuhusu kocha huyo hawezi kusema ndivyo alivyo sasa.

“Kwa sasa simjui, kipindi kile kila mtu alijua ni kocha mzuri na nsiyo maana alifanikiwa, anafanyaje kazi leo, mimi sijui, anaendeleaje hilo nalo sijui kwa kuwa siyo kocha wangu,” alisema Zlatan.

TEMEKE YAANZA NA MOTO AIRTEL RISING STARS

Na Mwandishi Wetu, DAR ES SALAAM
PAZIA la michuano Taifa ya soka ya vijana chini ya umri wa miaka 17 ya Airtel Rising Stars jana lilifunguliwa katika uwanja wa Kukumbukumbu ya Karume jijini Dar es Salaam ambapo timu ya wavulana ya Temeke ilitoa onyo kali kwa timu shiriki kwa kuifunga Kinondoni 4-1.
Mchezo huo ulitanguliwa na mechi ya wasichana kati ya Arusha na Lindi ambapo Arusha waliibuka na ushindi wa 2-0. Magoli ya Arusha yalifungwa na Eva Michael dakika ya 39 kwa njia ya penalti na pili likifungwa na Warda Alfonce dakika ya 60.
Mchezaji wa Arusha, Diana Mosses (kulia) akiwania mpira na beki wa Lindi , Neema Hashim katika mashindano ya vijana ya Airtel Rising Stars kwenye Uwanja wa Karume jijini Dar es Salaam jana

Katika mchezo wa Temeke na Kinondoni, Temeke walianza kwa kasi ya aina yake na kupeleka mashambuliazi ya mara kwa mara langoni mwa Kinondoni huku Kinondoni wakionekana kuzidiwa katika kila idara.
Temeke waliandika bao la kwanza kupitia kwa Ramadhan Kawambwa kaika dakika ya 14, kwa njia ya penati baada ya mchezaji wa Temeke kufanyiwa madhambi katika eneo la hatari. Goli hilo lilipokelewa kwa shangwa na mashabiki wa Temeke.
Temeke awalipata bao lao la pili kupitia kwa Abirahi Uihuro mnamo dakika ya 34 ambaye aligongeana mpira kwa uzuri na Ismail Kovu na kisha kumchambua kipa wa Kinondoni kwa umaridadi wa hali ya juu na kuukwamisha mpira huo kimiani.
Mohammed Mbegu aliifungia Temeke bao la tatu katika dakika ya 40 na kuzidi kuzamisha jahazi la Kinondoni ambao walinekana kama vile wamesimama wakati mchezo ukiendelea.
Rosea Mpoma aliwaliza kwa mara nyingine tena Arusha baada ya kuifungia Temeke bao la tano katika dakika ya 53 baada ya kuachia shuti kali na kuzama moja kwa moja wavuni.
Alikuwa ni Abirahi Uihuro tena, ambaye aliiandikia Temeka bao la nne mnamo dakika ya 28 ya kipindi cha pili baada ya kuunganisha krosi iliyochongwa na Mohammed Mbegu kutoka upande wa kushoto mwa uwanja na kuendeleza karamu ya magoli kwa Temeke.
Kinondoni walipata goli ya kufuta machozi mnamo dakika 36, likifungwa na Shaban Mangula baada ya mabeki ya Temeke kushindwa kuokoa mpira wa kona.
Michuano hiyo ya Airtel Rising Stars itaendelea kesho kwenye uwanja wa Karume jijini Dar es Salaam na kufikia tamati Jumapili, Septemba 11.