![]() |
| Christian Ronaldo |
Na salama ngale
Nyota Cristiano Ronaldo ametangazwa kuwa nahodha wa kikosi cha Real Madrid.
Anachukua
nafasi ya Alvaro Arbeloa aliyejiunga na West Ham United ya England.
Sasa anaungana na manahodha wengine watatu ambao ni Sergio Ramos, Pepe
na Marcelo.
Uamuzi
wa Madrid kumpa unahodha mshambuliaji huyo inaonekana ni sehemu ya
motisha kutokana na kufanya vizuri lakini ni kumfanya ajione hajapitwa
na mshambuliaji wa Barcelona, Lionel Messi ambaye pia ni kati ya
manahodha wane wa Barca.
Kumekuwa
na mjadala mkubwa katakana na Ronaldo kuwa nahodha wa Los Blanco,
wengine wakiamini imekuwa haraka sana na wengine wakiamini ni sahihi
kabisa.

No comments:
Post a Comment