Wednesday, 19 October 2016
Tennis: Kyrgios afungiwa kucheza wiki nane
Na Salama Ngale
Muaustralia Nick Kyrgios amefungiwa kwa wiki nane na kutozwa faini ya dola za kimarekani 25,000 kwa utovu wa nidhamu-ikiwa ni pamoja na kucheza ovyo wiki iliyopita michuano ya Shaghai Masters.
Nick mwenye miaka 21 amekuwa akigongesha mpira juu ya wavu mara kadhaa katika mchezo aliofungwa Mischa Zverev kwa seti 6-3 6-1 .Mchezaji huyo nambari 14 kwa ubora duniani ameomba radhi kwa tukio hilo na kusema atafanyia kazi wakati huu akiwa kifungoni.
Wiki iliyopita Muingereza Andy Murray alisema hafikirii kuwa faini pekee itakuwa adhabu tosha.
Mwaka 2015 Kyrgios alifungiwa siku 28 na faini ya dola 25,000 baada ya kutoa maneno ya kashfa kwa mpenzi wa Stan Wawrinka katika michuano ya kombe la Rogers.
TAKWIMU ZAMBEBA KIPA SIMBA, ASHIKILIA USUKANI WA KIPA BORA
![]() |
| VICENT |
Na salama Ngale
Kipa
wa Simba, Vincent Angban mpaka sasa ndiye aliyecheza mechi nyingi bila
kuruhusu bao ‘clean sheet’, akifanya hivyo kwenye michezo sita kati ya
tisa iliyocheza Simba huku akisimama golini mechi zote, sawa na dakika
810.
Muivory
Coast huyo aliyetoswa na Azam majaribioni mwanzoni mwa msimu kwa kile
walichosema kiwango chake ni hafifu, mpaka sasa amefanikiwa kuiweka
Simba kileleni mwa msimamo, huku akiwa ameruhusu mabao matatu tu katika
mechi tatu pekee.
Simba
inaungana na Yanga ambayo pia imeruhusu idadi hiyo ya mabao, ikiwa ni
idadi ndogo zaidi, lakini tofauti ni kwamba lango la Yanga limelindwa na
Deogratius Munishi ‘Dida’ na Ally Mustafa ‘Barthez’kwa nyakati tofauti.
Akizungumzia
clean sheet, Angban alisema ni jambo la furaha kwake na shukrani kwa
wachezaji wenzake pamoja na uwezo binafsi anayopigana kuhakikisha
anauonyesha awapo uwanjani.
“Ni
jambo zuri, lakini siku zote haya ndiyo matokeo ya mtu binafsi na timu
kwa ujumla. Siwezi kusema kuhusu ni clean sheet ngapi nifikishe kwa
sababu ninacheza kwa kujituma kwa ajili ya timu yangu ili iendelee
kufanya vizuri,” alisema kipa huyo.
Wednesday, 12 October 2016
POGBA APIGA BAO LA MWENDO KASI UFARANSA IKIILAZA UHOLANZI BAO 1-0
Holland (4-3-3): Stekelenburg,
Karsdorp, Bruma, van Dijk, Blind, Strootman, Wijnaldum (Dost 61), Promes
(Depay 16), Morishige (Willems 83), Klaassen, Janssen.
Subs not used: Zoet, Veltman, de Vrij, Kongolo, Clasie, Toornstra, Vilhena, De Jong, Vorm
Booked: Strootman, Morishige
France (4-2-3-1): Lloris, Sidibe,
Varane, Koscielny, Kurzawa, Pogba, Matuidi, Sissoko, Griezmann (Kante
90), Payet (Martial 66), Gameiro (Gignac 79).
Subs not used: Mandanda, Laporte, Fekir, Kimpembe, Cabaye, Digne, Corchia, Coman, Areola.
Goal: Pogba 30
Booked: Pogba
Argentina watandikwa Peru mechi ya kufuzu Kombe la Dunia
Mechi za Raundi ya
10 ya nchi za kanda ya Marekani ya Kusini chini ya Mwamvuli wa
Shirikisho lao CONMEBOL kusaka nchi 4 zitakazotinga moja kwa moja huko
Urusi Mwaka 2018 kwenye Fainali
Liverpool v Man Utd: Uteuzi wa refa Anthony Taylor wakosolewa
Mkuu wa zamani wa
marefa Uingereza Keith Hackett amekosoa uteuzi wa refa kutoka
Manchester Anthony Taylor kuwa mwamuzi wa mechi ya Ligi ya Premia kati
ya Liverpool na Manchester United.
Taylor huishi maili sita kutoka Old Trafford, na Hackett anaamini huenda hilo likasababisha madai wa kupendelea upande mmoja."Hakuna anayetilia sana uadilifu wake," Hackett alisema.
"Lakini je, kitu kikienda mrama? Itakuwa vigumu kwa baadhi kuvumilia."
Taylor hana uhusiano wowote na United lakini hushabikia klabu ya Ligi ya Taifa ya Kaskazini ya Altrincham.
Hackett anasema inashangaza ikizingatiwa kwamba Mark Clattenburg angepatikana siku hiyo ya Jumatatu.
Badala yake Clattenburg, ambaye ni shabiki wa Newcastle United, ataudumu kama mwamuzi wa nne mechi nyingine wikendi.
Tayari mashabiki wa Liverpool wameanza kulalamika mitandao ya kijamii kuhusu uteuzi wa Taylor.
Subscribe to:
Posts (Atom)







